Wizara ya Afya ya Afrika Kusini imetangaza kuwa, idadi ya watu walioambukizwa kirusi hatari cha corona nchini humo jana ilipanda hadi watu 38 kutoka 24 waliokuwa wameambukizwa kirusi hicho hadi juzi Ijumaa.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, watu 14 waliokumbwa na ugonjwa wa COVID-19 wameongezeka katika kipindi cha siku moja nchini Afrika Kusini.

Huku hayo yakiripotiwa, idadi ya walioambukizwa kirusi cha corona imeongezeka mara mbili pia nchini Morocco baada ya nchi hiyo kuripoti kesi nyingine 9 za maambukizi ya kirusi hicho jana Jumamosi. Hadi kufikia jana, watu 17 walikuwa wameshaambukizwa corona nchini humo kwa mujibu wa wizara ya afya ya Morocco.

Kati ya kesi hizo mpya za maambukizi ya kirusi cha corona, imo moja ya mtu wa ndani ya Morocco kwenyewe wakati kesi zilizobakia ni za watu waliotoka katika nchi za Ulaya za Uhispania, Italia na Ufaransa.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...