Na Amiri kilagalila,Njombe
Wakati baadhi ya wanawake wakiungana mkoani Njombe kuadhimisha siku ya wanawake duniani inayotarajiwa kufikia kilele chake hapo machi 8 mwaka huu,wananchi wametakiwa kuacha tabia ya kukataa kujitokeza kutoa ushahidi mahakamani ili kukamilisha upelelezi utakaosaidia kupunguza msongamano wa mahabusu na wafungwa gerezani.
Kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Njombe katibu tawala wilaya bwana Emmanuel George baada ya kufika katika gereza la wilaya ya Njombe (Mpechi) na kukabidhi baadhi ya msaada wa vitu muhimu kama mafuta huku akiongozana na wanawake wanaoendelea kufanya shughuli mbalimbali kuelekea siku ya wanawake duniani amesema kuwapo kwa msongamano mkubwa wa mahabusu na wafungwa unasababishwa na jamii kuto jitokeza kutoa ushahidi wakati wa kesi mahakamani.
“Njombe watu hawatoi ushirikiano ili kesi ziishe haraka lakini ni rai yangu kutoa ushahidi wa haraka ili kupunguza idadi ya mahabusu kwenye magereza yetu lakini niwapongeze uongozi wa gereza kwa kuwatengeneza hawa watu kisaikolojia”alisema Emmanuel George
Lilian Nyemele ni katibu tarafa wa Njombe mjini aliyeongozana na wanawake wenzake kutoa misaada mbalimbali huku akisema kupitia muendelezo wa kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani anasema wameguswa na kundi la mahabusu wanawake na kuona umuhimu wa kwenda kuwashika mkono.
Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa gereza la wanawake Njombe askari Theresia Kiswaga anasema kitendo kilichofanyika na wanawake hao kinafaa kuigwa katika jamii kwani vitu walivyowapa mahabusu na wafungwa vitawasaidia sana kuwapunguzia ukali wa maisha ndani ya gereza hilo.
“Lakini pia tunaendelea kutoa wito kuendelea kututembelea sio tu kusubiri sherehe,tunaomba hata siku ya jumamosi au jumapili kuja kuwaona hawa ndugu zetu na hata siku za sikuku za kitaifa,vifaa vilivyotolewa vitakuwa na msaada kwetu kwa mfano maziwa kwa ajili ya watoto hapa sisi hatuna mifugo lakini mmetuletea maziwa tunashukuru”alisema Thelesia Kiswaga
Kwa upande wake mkuu wa gereza la wilaya ya Njombe SSP  Charles  Mhinga amekiri kuwa misaada hiyo ni upendo tosha uliopo baina ya wanawake na ndugu zao waliopo katika mazingira magumu ya gerezani.
“Nimefarijika sana kwa misaada hii ambayo akina mama kwa umoja wao wamekuja kuwasilisha kwa wamama wenzao ambao wapo katika mazingira haya,uhitaji upo lakini sisi tunashukuru kwa hili”alisema Cherls Mhina
Miongoni mwa misaada iliyotolewa na akina mama mkoani katika gereza hilo ni pamoja na Sabuni,taulo za kike,ndala ,mafuta na hata mavazi mabali mbali
bado shughuli mbalimbali zinaendelea kufanyika na wanawake hao ikiwemo kufanya maonesho ya bidhaa katika viwanja vya turbo mjini Njombe huku wito ukitolewa kwa jamii kujitokeza kuwaunga mkono wanawake katika nyanja mbalimbali. 
 Baadhi ya viongozi na wanawake wakisalimiana baada ya kufika gereza la mpechi kwa ajili ya kutoa misaada
 Akina mama na viongozi wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Magereza mara baada ya kuwatembelea mahabusu na wafungwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...