Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Salum Manyata amewahasa wataalamu wa kutoa dawa za usingizi nchini kuwa wana jukumu kubwa la kuboresha utoaji wa huduma wa dawa za usingizi kwa kina mama wajawazito wakati wa upasuaji ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza wakati wa utoaji huduma hiyo.
Dkt. Manyata ameyasema leo wakati akifungua mafunzo elekezi ya utoaji dawa za usingizi salama wakati wa upasuaji kwa kina mama wajawazito yanayofanyika jijini Mbeya kwa siku tatu na kushirikisha wataalamu kutoka vituo vya afya na hospitali zilizoko Nyanda Juu kusini.
Amesema kuwa ni vema washiriki hao kutumia fursa walioipata ya mafunzo hayo ya kujengewa uwezo ili kutekeleza yale ambayo wameyapata kwa kutoa huduma salama na sahihi.
Dkt. Manyata amewaasa wataalamu hao kupeleka mrejesho wa maswala mbailimbali mapya waliyoyapata kwa wengine katika vituo vyao watakaporejea ili kuhakikisha taratibu zote zinasimamiwa vizuri.
Mafunzo hayo yanatolewa na wakufunzi kutoka ndani na nje ya nchi na kushirikisha wataalam 35 wa dawa za usingizi kutoka Nyanda za Juu Kusini na kufadhiliwa na Chama cha Madaktari Bingwa wa dawa za usingizi duniani (WFSA) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa dawa za usingiizi Tanzania (SAFE) kwa malengo ya kuwajengea uwezo watoa huduma ya dawa ya usingizi katika vituo vya afya na hospitali vile vile kupunguza vifo vya kina mama wajawazito wakati wote wa upasuaji.
Dkt. Manyata ameyasema leo wakati akifungua mafunzo elekezi ya utoaji dawa za usingizi salama wakati wa upasuaji kwa kina mama wajawazito yanayofanyika jijini Mbeya kwa siku tatu na kushirikisha wataalamu kutoka vituo vya afya na hospitali zilizoko Nyanda Juu kusini.
Amesema kuwa ni vema washiriki hao kutumia fursa walioipata ya mafunzo hayo ya kujengewa uwezo ili kutekeleza yale ambayo wameyapata kwa kutoa huduma salama na sahihi.
Dkt. Manyata amewaasa wataalamu hao kupeleka mrejesho wa maswala mbailimbali mapya waliyoyapata kwa wengine katika vituo vyao watakaporejea ili kuhakikisha taratibu zote zinasimamiwa vizuri.
Mafunzo hayo yanatolewa na wakufunzi kutoka ndani na nje ya nchi na kushirikisha wataalam 35 wa dawa za usingizi kutoka Nyanda za Juu Kusini na kufadhiliwa na Chama cha Madaktari Bingwa wa dawa za usingizi duniani (WFSA) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa dawa za usingiizi Tanzania (SAFE) kwa malengo ya kuwajengea uwezo watoa huduma ya dawa ya usingizi katika vituo vya afya na hospitali vile vile kupunguza vifo vya kina mama wajawazito wakati wote wa upasuaji.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Salum Manyata akitoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo kwa wataalamu wa kutoa dawa za usingizi wa vituo vya afya na hospitali Nyanda za juu Kusini katika ukumbi wa Usungilo jijini Mbeya
Wataalam wa dawa za usingizi wakitoa elimu kuhusu namna ya kutoa huduma ya dawa za usingizi iliyo salama na sahihi kwa washitiri waliohudhuria mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki vituo vya afya na hospitali wa nyanda za juu kusini wakifwatilia mada
Wakufunzi Madaktari Bingwa wa Dawa za Usingizi katika picha ya pamoja na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Salum Manyata.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Salum Manyata katika Picha ya pamoja na Viongozi Waratibu wa mafunzo ya huduma salama na sahihi ya dawa za usingizi na washitiri kutoka vituo vya Afya na Hospitali wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...