Na Zainab  Nyamka, Globu ya Jamii

Mkurugenzi wa Lebo ya Kings Music Records Ali Saleh Kiba amewataka mashabiki wa muziki kukaa tayari kumpokea msanii wake mpya Tommy Flavour.

Ni takribani siku tatu zimepita toka msanii huyo kupoteza wasanii wake wawili Cheedy na Killy tz walioamua kuondoka kwenye lebo ya Kings Music Records.

Akiandika katika mtandao wake wa Kijamii, Ali Kiba amesema kuwa Ijumaa hii atamtambulisha msanii mpya chini ya lebo ya Kings Music Records na kuwataka mashabiki wake wajiandae kumpokea.

"It’s official kwamba this Friday @kingsmusicrecords inamtambulisha rasmi @tommyflavour kwenye music industry. Kuwa wa kwanza kusikiliza na kuangalia kazi zake mpya kwa subscribe kwenye Youtube Channel ya Tommy Flavour"

Mbali na hilo, Ali Kiba anatarajia kuwa msanii wa pili kufanya tamasha la Live wakiliita Hima TVE Chill and Feel the Vibe kupitia kituo cha Luninga cha ETV ambao ataimba na kuwaburudisha mashabiki wake wakiwa nyumbani.

Ali Kiba kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya wa Dodo unaofanya vizuri kwenye mitandao mbalimbali akiwa amemshirikisha msanii na mwanamitindo Hamisa Mobeto kama Video Vixen.

 Msanii wa kwanza kufanya tamasha la Live alikua ni Nandy na aliweza kuvalishwa pete ya Uchumba na rafiki yake wa siku nyingi msanii mwenzake Billinas.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...