Pichani ni Muonekano wa Kisiwa cha Musira na Bandari ya Bukoba kama palivyonaswa na Kamera yetu
Pichani ni baadhi ya abiria na wananchi mbalimbali wakinawa Mikono eneo la Stendi ya Bukoba wakati wanapoingia na kutoka katika kituo cha Mabasi Bukoba, lengo ni kuendelea kuchukua Tahadhari ya Corona.
Pichani ni Mtumishi wa Idara ya Afya akiendelea na majukumu yake ya kuwapima wasafiri wanaoingia Mkoani Kagera, kutokea maeneo mbalimbali pindi wanapoteremka katika Mabasi.
Pichani ni katikati ya Manispaa ya Bukoba hali ya usafi ikizidi kuimarishwa, hapakuna msongamano wa watu licha ya kuwa Leo ni mwisho wa Wiki.
Pichani ni Muonekano wa Kituo cha Mabasi Bukoba shughuli mbalimbali zikiendelea na Tahadhari ya Ugonjwa wa Corona ikizidi kuchukuliwa.
Pichani
ni kipande cha Barabara Mtaa wa Shoe maarufu Bukoba Club katika hatua
ya Mwisho wakati Daraja la eneo hilo likiwa katika hatua za kukamilika
Pichani ni shughuli za usafi zikiendelea mitaa mbali mbali ndani ya Manispaa ya Bukoba
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...