*****************************
NA MWAMVUA MWINYI,BAGAMOYO
Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Kawambwa amekabidhi pikipiki tatu kwa kikundi cha waendesha bodaboda kilichopo kitongoji cha Benki kata ya Dunda ,Huku akiwaasa wajasiriamali kutopuuzia kujiunga vikundi kwani vinasaidia kupata fursa mbalimbali kirahisi.
Pikipiki hizo ambazo zimenunuliwa kutokana na mkopo uliotolewa na halmashauri ya Bagamoyo kwa vijana, zimekabidhiwa kwa kikundi hicho kinachojulikana kwa jina la Umoja wa Madereva wa Bodaboda Stendi Geti namba 4, (UMABOS G4).
Akizungumza wakati wa kukabidhi pikipiki hizo, Mbunge huyo wa jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa aliwapongeza vijana hao kwa kuchangamkia fursa na kwamba wao ni mfano wa kuigwa.
Alisema Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Magufuli inawajali wananchi wa hali ya chini ndiomana kila halmashauri kuna mfuko kwaajili ya vijana, kinamama na walemavu ambapo makundi hayo hukopeshwa na kurejesha bila ya riba.
Alisema serikali haiwezi kumpa fedha mtu mmoja mmoja lakini inatoa kwa vikundi ili iwe rahisi kuwahudumia watu wengi wenye uhitaji kwa wakati mmoja. 

Kwa upande wake, Diwani wa kata ya Dunda, Dickson Makamba aliwapongeza vijana hao na kusema kuwa hao ni vijana wa mfano katika kata yake. 

Alisema kikundi hicho hakina muda mrefu toka kuanzishwa kwake lakini mafanikio yake ni makubwa katika kipindi kifupi ukilinganisha na vikundi vingine ambavyo vina muda mrefu. 

Awali akisoma taarifa ya kikundi Katibu wa kikundi hicho Abdalla Shabani Jongo alisema malengo yao ni kupata pikipiki tano na kwamba mpaka sasa wamefanikiwa kupata pikipiki tatu .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...