Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
OLIVE Veronisi (93) mkazi wa Pittsburgh Pennsylvania ameteka mitandao ya kijamii baada ya picha yake akiwa na kopo la bia na bango lenye ujumbe wa "Nahitaji bia zaidi" kusambaa na kupendwa na  watu wengi zaidi.

Mwanamke  alionekana kutokea dirisha la nyumba yake akitekeleza agizo la kutotoka nje (lockdown) ikiwa ni sehemu ya kupambana na virusi vya Corona (Covid -19) vilivyosambaa kote duniani.

Imeelezwa kuwa picha hiyo ambayo ilichukuliwa na jamaa zake imetazamwa zaidi ya mara milioni 4 katika mtandao wa Facebook jambo lililopelekea kampuni ya vinywaji ya Morson coors kumpa alichokuwa anahitaji.

Mapema jumatatu Olive alipokea kopo150 za bia kutoka Molson Coors ambapo msemaji wa Molson Coors Darren Rovell amesema kuwa baada ya kuona ujumbe huo waliamua kuungana na mtu aliyeleta tabasamu usoni mwa watu wakati wa janga hili la Corona na wamemshukuru Olive kwa kuwa shabiki wa kinywaji cha Coors Light.

Mara baada ya kupokea zawadi hiyo Olive alikuja kivingine kwa kushika bango lililosomeka "Nimepata bia zaidi."

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...