Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MIAKA saba iliyopita Waziri mkuu wa Ireland  Leo Varadkar aliacha fani yake ya udaktari na kuingia kwenye siasa na leo amerudi katika fani yake ya awali akihudumu kama daktari ikiwa na sehemu ya kuisaidia nchi dhidi ya mlipuko wa virusi vya Corona (Covid -19) ambapo hadi sasa taifa hilo lina visa 4994 Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na chuo kikuu cha Johns Hopkins siku ya Jumatatu.

Varadkar aliyehudumu katika sekta ya afya kama daktari kwa miaka saba aliondolewa katika usajili huo mwaka 2013 kabla ya kujisajili upya mwezi Machi.

Mapema mwezi Machi mwaka huu waziri wa afya nchini humo Simon Harris alieleza mkakati wa Wizara hiyo katika Kupambana na mlipuko wa virusi hivyo na kuelekeza ujumbe wa "Nchi yako inakuhitaji" kwa Waziri mkuu huyo.

Varadkar atahudumia wagonjwa mara moja kwa wiki huku ikielezwa kuwa usajili wake umelenga kuwasaidia wananchi hata kwa kiasi kidogo.

Varadkar Leo akiwa Waziri mkuu na daktari ametokea kwenye familia ya watatibu ambapo baba yake ni daktari na mama yake ni muuguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...