HAZINA: MKURUGENZI Mtendaji Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Nyamajeje Caleb Weggoro, akipokea Kitabu cha MAKING AFRICA WORLD'S LARGEST ECONOMY kutoka kwa mwandishi wake, Derek Murusuri, jijini Arusha mwishoni mwa wiki hii.
Dkt. Nyamajeje alikuwa anawakilisha mataifa nane (8) ya Afrika katika Bodi ya Wakurugenzi ya AfDB.
Nchi hizo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Ethiopia, Eritrea, Seychelles na Sudan ya Kusini.
Dkt. Nyamajeje ambaye amefurahishwa na ujio wa kitabu cha MAKING AFRICA WORLD'S LARGEST ECONOMY, amesema kwamba ili kuhamasisha maendeleo ya Afrika, ni muhimu kwa waafrika kuandika habari zetu wenyewe (telling our own stories) na kuona fahari kutengeneza mashujaa wetu ili kuimarisha ujenzi wa jamii imara barani zitakazojiletea maendeleo zenyewe badala ya kuendelea kuyategemea mataifa wahisani.
Dkt Nyamajeje ambaye pia aliwahi kuwa Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye masuala ya Uchumi na Utangamano wa Mataifa ya Afrika, vilevile alikuwa miongoni mwa viongozi walioisuka upya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Amewashauri watanzania kujenga utamaduni wa kuandika na kusoma vitabu ili kutunza na kuijua historia yao, ambayo ni muhimu katika kuhifadhi urithi wetu.
Dkt. Nyamajeje alikuwa anawakilisha mataifa nane (8) ya Afrika katika Bodi ya Wakurugenzi ya AfDB.
Nchi hizo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Ethiopia, Eritrea, Seychelles na Sudan ya Kusini.
Dkt. Nyamajeje ambaye amefurahishwa na ujio wa kitabu cha MAKING AFRICA WORLD'S LARGEST ECONOMY, amesema kwamba ili kuhamasisha maendeleo ya Afrika, ni muhimu kwa waafrika kuandika habari zetu wenyewe (telling our own stories) na kuona fahari kutengeneza mashujaa wetu ili kuimarisha ujenzi wa jamii imara barani zitakazojiletea maendeleo zenyewe badala ya kuendelea kuyategemea mataifa wahisani.
Dkt Nyamajeje ambaye pia aliwahi kuwa Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye masuala ya Uchumi na Utangamano wa Mataifa ya Afrika, vilevile alikuwa miongoni mwa viongozi walioisuka upya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Amewashauri watanzania kujenga utamaduni wa kuandika na kusoma vitabu ili kutunza na kuijua historia yao, ambayo ni muhimu katika kuhifadhi urithi wetu.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...