Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Tandahimba wameridhia baadhi ya fedha za miradi ya maendeleo kutumika katika shughuli za kupambana na ugonjwa wa Corona (Covid - 19)
Hatua hiyo wamefikia katika kikao Cha Baraza ambalo limefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Tandahimba
Aidha madiwani wamesema kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na Wilaya dhidi ya kuhakikisha wananchi wao pia watachangia fedha ambazo zitasaidia kununulia vifaa mbalimbali vya kujikinga na uginjea wa Corona
Mbali na Hilo madiwani hao wameomba Wakala wa Barabara vijijini na mijini (Tarura) kutengeneza baadhi ya barabara ambazo kwa Sasa zimejifunga
"Tarura watuchongee Barabara maeneo yetu mengi ya wilaya sasa hivi hayapitiki ,walichukue hili Kama dharura hasa katika kipindi hiki Cha Corona,ubovu wa miundombinu ya barabara ni tatizo ambalo limeanza miaka miwili hii awali Barabara zote zilikuwa zinapitika kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwakuwa zilikuwa zinachongwa ,"amesema diwani wa MihutaHamis Mfaume.


Madiwani wakipuliziwa dawa kabla ya kikao Cha baraza

Hatua hiyo wamefikia katika kikao Cha Baraza ambalo limefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Tandahimba
Aidha madiwani wamesema kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na Wilaya dhidi ya kuhakikisha wananchi wao pia watachangia fedha ambazo zitasaidia kununulia vifaa mbalimbali vya kujikinga na uginjea wa Corona
Mbali na Hilo madiwani hao wameomba Wakala wa Barabara vijijini na mijini (Tarura) kutengeneza baadhi ya barabara ambazo kwa Sasa zimejifunga
"Tarura watuchongee Barabara maeneo yetu mengi ya wilaya sasa hivi hayapitiki ,walichukue hili Kama dharura hasa katika kipindi hiki Cha Corona,ubovu wa miundombinu ya barabara ni tatizo ambalo limeanza miaka miwili hii awali Barabara zote zilikuwa zinapitika kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwakuwa zilikuwa zinachongwa ,"amesema diwani wa MihutaHamis Mfaume.


Madiwani wakipuliziwa dawa kabla ya kikao Cha baraza


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...