Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Tandahimba wameridhia baadhi ya fedha za miradi ya maendeleo kutumika katika shughuli za kupambana na ugonjwa wa Corona (Covid - 19)

Hatua hiyo wamefikia katika kikao Cha Baraza ambalo limefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Tandahimba

Aidha madiwani wamesema kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na Wilaya dhidi ya kuhakikisha wananchi wao pia watachangia fedha ambazo zitasaidia kununulia vifaa mbalimbali  vya kujikinga na uginjea wa Corona

Mbali na Hilo madiwani hao wameomba Wakala wa Barabara vijijini na mijini (Tarura) kutengeneza baadhi ya barabara ambazo kwa Sasa zimejifunga

"Tarura watuchongee Barabara  maeneo yetu mengi ya wilaya sasa hivi hayapitiki ,walichukue hili Kama dharura hasa katika kipindi hiki Cha Corona,ubovu wa miundombinu ya barabara ni tatizo ambalo limeanza miaka miwili hii awali  Barabara zote zilikuwa zinapitika kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwakuwa zilikuwa zinachongwa ,"amesema diwani wa MihutaHamis Mfaume.



Madiwani wakipuliziwa dawa kabla ya kikao Cha baraza


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...