Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MCHORAJI na mwongozaji wa vibonzo vya panya (Tom) na paka (Jerry) Eugene Merrill Deitch amefariki dunia ghafla akiwa na umri wa miaka 95 huko nyumbani kwake Prague,  mchapishaji wake Peter Himmel ameieleza The Associated Press.

Imeelezwa kuwa Eugene aliyezoeleka kuitwa Gene ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya Oscar alifariki dunia ghafla siku ya Alhamisi usiku akiwa katika makazi yake.

Gene ameongoza sehemu zipatazo kumi na tatu za vibonzo vipendavyo na watoto ulimwenguni kote maarufu kama "Tom and Jerry" pamoja na baadhi  kutoka mfululizo wa visa vya Popeye.

Gene aliwahi kufanya kazi kama msanifu wa anga la Amerika Kaskazini kabla ya kuandikishwa jeshini na kuingia katika mafunzo ya majaribio ya urubani na mwaka 1959 alihamia katika makazi yake huko Prague.

Aidha filamu yake ya Munro ilishinda tuzo filamu bora ya picha na michoro mwaka 1960 na alichaguliwa mara mbili katika uteuzi wa kipengele cha namna hiyo mwaka 1964 kwa filamu za Nudnik na How to Avoid Friendship.

Awali Gene alitengeneza mfululizo wa filamu ya visa ya  Tom  ambapo Sidney's Family Tree iliteuliwa katika tuzo Academy mwaka 1958.

Gene alikua akiishi na mkewe na watoto wake wa kiume watatu kutoka ndoa yake ya kwanza ambao wote ni wahusika katika vibonzo.

Mashibiki wengi wameeleza kusikitishwa na kifo hicho ambapo kurasa nyingi za Twitter zimejaa Salamu za rambirambi kufuatia kifo hicho ambapo wengi wameeleza kuwa Gene alikuwa zaidi ya Tom na Jerry na atakumbukwa daima kupitia vibonzo hivyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...