Marekani imerekodi vifo vingi vya ugonjwa wa corona kwa siku huku watu 1,736 wakifariki siku ya Jumanne.

Idadi hiyo inaweka watu waliofariki kutokana na virusi hivyo nchini humo kufikia 12,722 kulingana na data za chuo kikuu cha Johns Hopkins.

Marekani ina wagonjwa 398,000 wa virusi hivyo waliothibitishwa , ikiwa ndio idadi kubwa zaidi duniani .

Visa vyote duniani vimepita watu milioni 1.4. Hatahivyo wakati wa mkutano na vyombo vya habari , rais Donald Trump alisema kwamba Marekani huenda inafikia kilele cha 'upinde'.

Wakati huohuo Mji wa Wuhan nchini China ambapo maambukizi yalianza umekamilisha amri yake ya kutengwa kwa wiki 11.

Takwimu mpya zilizotangazwa siku ya Jumanne zimepita rekodi ya awali iliokuwa na vifo 1,344 kwa siku nchini Marekani ambapo ilitokea tarehe 4 mwezi Aprili.

Idadi ya vifo inatarajiwa kupanda huku baadhi ya majimbo yakiwa bado hayajatoa takwimu zao za jumla.

Familia ya msanii wa Marekani John Prine imethibitisha kwamba msanii huyo alifariki kutokana na virusi hivyo vya corona.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...