Papa Francis amewataka watu kutosalimu amri kwa uoga wa virusi vya corona, na kuwataka kuwa "wajumbe wa uhai wakati wa kifo".

Kiongozi huyo wa kanisa katoliki alizungumza wakati wa sherehe za pasaka Jumamosi, katika kanisa la St Peter's Basilica ambalo lilikuwa na watu wachache.

Waumini wa Kikatoliki bilioni 1.3 kote duniani wana fursa ya kufuatilia ibada ya moja kwa moja mtandaoni.

Marufuku ya watu kutokutoka majumbani bado inaendelezwa katika maeneo mbalimbali nchini Italia ambako kumeathiriwa vibata na janga la Corona.

Waziri Mkuu wa Italia Giuseppe Conte alimsifu Papa kwa kuonyesha kuchukua majukumu yake kwa tahadhari baada ya kuadhimisha ibada ya pasaka bila ya mkusanyiko wa waumini.

Wakristo kote duniani wanasherehekea sikukuu ya pasaka, moja ya sikukuu muhimu katika kalenda ya Kikikristo licha ya hatua zilizochukuliwa katika nchi nyingi duniani zilizosababisha mamilioni ya watu kusalia majumbani

Makasisi wengi wanaendesha ibada zao makanisani bila waumini kukusanyika.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...