Na Mwandishi wetu Mihambwe

Leo Jumatatu Aprili 6, 2020 Afisa Tarafa Mihambwe Emmanuel Shilatu amewashukuru Wananchi wa Tarafa ya Mihambwe kwa kuitikia vyema wito wa Serikali wa kupambana na ugonjwa wa Covid 19 unaosababishwa na kirusi Corona.

Gavana Shilatu ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kukagua maeneo mbalimbali kuona namna gani Wananchi wanajikinga na ugonjwa wa virusi vya Corona ambapo alikuta Watu wengi wamezingatia somo la kunawa kwa kuweka ndoo yenye maji pamoja na sabuni ambapo Wananchi wananawa mara kwa mara maji yanayotiririka.

“Kiukweli inatia faraja sana kuona Wananchi wanaungana na Serikali yao kupambana na Corona kwa nguvu moja. Kwenye mapungufu madogo madogo tuliyoyaona tumewaelimisha zaidi. Nimewasisitiza waendelee kusikiliza na kufuata maelekezo ya Wataalamu wa Afya juu ya namna ya kujikinga na ugonjwa huu.” Alisema Gavana Shilatu.

Kwenye ziara hiyo Gavana Shilatu aliambatana na Watendaji kata na vijiji, Maafisa afya pamoja na Viongozi wa Serikali ya Halmashauri ya Kijiji kutembelea maeneo yanayotoa huduma kwa jamii kama vile kwenye maduka na masoko.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...