Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akitoa maelekezo maalum leo Mei 04, 2020  katika kikao kazi cha Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza, Boharia Mkuu wa Jeshi ambapo Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akiwa meza kuu pamoja na Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo akiwemo Kamishna wa Magereza anayeshughuliika na Utawala na Rasilimali watu, Uwesu Ngarama(kulia). Kushoto ni Kamishna wa Magereza anayesimamia Divisheni ya Urekebu, Mhandisi Tusekile Mwaisabila leo Mei 04, 2020 wakifuatilia kikao kazi cha Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza pamoja na Boharia Mkuu wa Jeshi hilo.
Baadhi ya Maafisa walioteuliwa kushika nyadhifa malimbali katika Jeshi la Magereza wakiwemo wakuu wa magereza wakifuatilia kikao kazi cha maelekezo ambacho kilikuwa chini ya Uenyekiti wa Kamishna Jenerali wa Magereza, leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma. Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi hilo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee leo Mei 04, 2020 akizungumza na baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Magereza walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Jeshi hilo wakiwemo wakuu wa magereza, Boharia Mkuu wa Jeshi ambapo Jenerali Mzee amewataka kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo Agenda ya mabadiliko ndani ya Jeshi la Magereza.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee akizungumza na Maafisa kutoka Vyuo vya Mafunzo Zanzibar(kulia) ambao wametembelea Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Tanzania Bara, leo Mei 04, 2020  jijini Dodoma (Picha zote na Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...