Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

HADI sasa Lesotho haijatangaza kisa cha maambukizi ya homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19) licha ya majirani zao Afrika kusini kuwa na kesi za Covid-19 zaidi ya elfu saba na vifo zaidi ya mia moja, pia Lesotho inakua nchi pekee kati nchi 54 barani Afrika ambayo haijaripoti maambukizi ya virusi hivyo ila nchi hiyo imeendelea kuchukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kufunga, mipaka, vyuo, shule pamoja na shughuli nyingine zinazoleta mkusanyiko wa watu.

Baadhi ya wachambuzi wameeleza kuwa nchi hiyo imekua ikiishi kwa tahadhari kubwa kutokana na maambukizi ya kiwango cha juu ya Virusi vya UKIMWI (VVU) vilivyoikumba nchi hiyo katika miaka ya themanini na mwaka 1986 kutangazwa kuwa ni janga la taifa ambalo lilipelekea nchi hiyo kuwa ya pili duniani kwa kiwango kikubwa cha maambukizi wa VVU.

Wataalamu wameeleza kuwa huenda sababu ya nchi hiyo kutokupata maambukizi ni kutokana na maeneo mengi ya nchi hiyo yenye milima kutofikika na nusu ya idadi ya watu wanaishi vijijini hivyo kuweka vizuizi ni rahisi kuliko nchi zenye idadi kubwa ya watu (ikumbukwe Lesotho ina watu wapatao milioni mbili,)  Afrika kusini ambayo ipo karibu zaidi na Lesotho imeathirika na Covid-19 na vizuizi vilivyowekwa vinazidi kuwasaidia majirani hao.

Nchini Lesotho asilimia 25 au mtu mmoja kati ya wanne anaishi na maambukizi ya VVU, huku nusu ya vijana  300,000 ambao ni wanawake (miaka 15 -25) wanaishi na maambukizi hayo na zaidi ya yatima 200,000 ni zao la VVU, hii ni kwa mujibu wa Shirika la Afya duniani (WHO.)

Kutokana na maambukizi hayo tahadhari nchini humo zimekuwa zikitolewa kila siku na hasa ni kwa kuwahimiza wananchi katika matumizi sahihi ya kondomu pamoja na kupima afya zao huku kundi la vijana likielezwa kuwa hatarini zaidi katika janga hilo kwani vijana wengi wanaoingia katika mahusiano hawajui hali za wenza wao.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa mwaka 2018 inaonesha kuwa  watu 340,000 wanaishi na VVU Lesotho huku watu 6,100 wakifa kwa virusi hivyo.

Mapema wiki iliyopita waziri mkuu wa nchi hiyo Thomas Thabane alihutubia taifa na kueleza kuwa Serikali italegeza vizuizi vilivyowekwa mwezi jana ikiwa ni pamoja na kuruhusu uendeshaji wa biashara ila kwa muda maalumu, kufungua kwa shule na vyuo pamoja na ofisi za umma ambazo zitafunguliwa na kufungwa kwa muda uliopangwa.

Thabane aliwataka wananchi kuendelea kuvaa barakoa pamoja na kufuata sheria zinazotolewa na Wizara ya afya pamoja na Shirika la Afya Duniani.

Hata hivyo alieleza kuwa mipaka ya nchi hiyo itaendelea kufungwa wakati huu ambao nchi hiyo inapambana katika kuzuia kuenea kwa virusi hivyo.

Ikumbukwe kuwa licha Thabane Thomas kuongoza mapambano dhidi ya virusi vya Corona nchini humo Alhamisi ya wiki iliyopita alitangaza kuachia madaraka mwisho wa mwezi Julai  huku ikielezwa kuwa ni maamuzi ya hiari kutokana na umri wake lakini wachambuzi wa masuala nchini humo wameeleza kuwa kuachia madaraka hayo kunatokana kesi ya mauaji ya mkewe ambayo inamkabili yeye na mke wake Maesaiah Thabane aliyemuoa miezi miwili baada ya kifo cha mke wake wa kwanza Lipolelo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...