NA MWANDISHI WETU.

MTANDAO wa Wanawake Laki Moja  (100,000  WOMEN) wenye lengo la kuunganisha na Wanawake, kupambana na Ukatili wa Kijinsia na Umasikini hapa nchini umetoa pongezi kwa akina Mama wote walio mstari wa mbele kwenye mapambano dhidi ya virusi vya Corona.

Pongezi hizo zimetolewa leo ambayo ni siku ya Kina Mama (Mother's Day )  ambapo wamekuwa mstari wa mbele katika mapambano.

"WanawakeLakiMoja tunawapongeza kina Mama wote wa Tanzania na duniani kwa ujumla.Kazi kubwa wanazozifanya za kubeba majukumu ya familia na jamii" ilisema taarifa yao.

Mtandao huo ambao unafanya kazi Tanzania nzima. Kwa sasa upo katika Mikoa 21.

Mtandao huo ulianza mapema mwezi Januari 2020 na makao makuu yake ni Jijini Mwanza.

Katibu wa Mtandao huo, Madam Josephine Ngoda alieleza kuwa, Wanawake wenye lengo la kujiunga na mtandao huo wanakaribishwa.

"Wanawake tunawakaribisha.  Unapaswa kujitambulisha pahala ulipo na unafanya nini na ujumbe kwa wanawake kisha kupakia ( ku post) katika mitandao yetu ya kijamii ikiwemo facebook na Instagram
 Facebook@wanawakelakimoja na Instagram@wanawakelakimoja"
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...