Na Karama Kenyunko Michuzi TV 
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema Mbunge wa Kawe, Halima Mdee anayekabiliwa na kesi ya uchochezi kwa kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya Rais John Magufuli anayo kesi ya kujibu.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ametoa uamuzi huo leo Mei 28, 2010 wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutolewa uamuzi.

Hatua hiyo imekuja baada ya Februari 20, mwaka huu upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao kufuatia mashahidi watatu waliofika mahakamani hapo kutoa ushahidi ambao leo mshtakiwa Mdee ameonekana na kesi ya kujibu.

Hata hivyo Mdee kupitia wakili wake Hekima Mwasipo amesema mteja wake atajitetea kwa kiapo na atakuwa na mashahidi watano.

Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa Julai 3,2017 katika Makao Makuu ya Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni, Mdee anadaiwa kutamka maneno dhidi ya  Rais John Magufuli kuwa  “anaongea hovyohovyo , anatakiwa  afungwe breki”  na kwamba kitendo ambacho kingeweza  kusababisha uvunjifu wa amani.  

Mdee alifikishwa mahakamani hapo Julai 10, 2017 na yupo nje kwa dhamana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...