Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

NCHINI Ecuador miili ya waathirika wa virusi vya Corona imeendelea kuzagaa mitaani huku tahadhari zaidi ikitolewa dhidi kuenea kwa virusi hivyo.

Baadhi ya wachunguzi  wameonekana katika moja ya mitaa wakichunguza maiti ya mwanaume wa miaka 65 aliyedaiwa kuambukizwa COVID-19 katika mji mkuu wa nchi hiyo Quito siku ya Jumanne na baadaye wafanyakazi wa wazishi walifika na kumweka kwenye jeneza na kumsafirisha, Dailymail imeripoti.

Ecuador ina zaidi ya kesi 31,000 zilizothibitishwa za Covid-19 pamoja na vifo zaidi ya1,569.

Katika ukanda huo Ecuador ni nchi ya tatu kuathirika zaidi baada ya Brazil yenye  vifo 7,921 na kesi 114,715 na Mexico ambayo imerekodi vifo 2,271 na kesi 26,025.

Wataalam wameeleza kuwa gonjwa hilo litazidi kuenea kwa kasi katika  ukanda wa Latin Amerika katika siku zijazo.

Nchi kadhaa, ikiwemo Ecuador, Colombia na Jamhuri ya Dominika, wameongeza hatua  za kuchukua tahadhari zaidi ikiwa ni sehemu ya kupambana na janga hilo.

Ikumbukwe kuwa tangu Ecuador itangaze kisa cha kwanza Februari 29, ukanda wa pwani wa Guyas ulikuwa na maambuki 4,000 sawa na asilimia 70 huku Guayaquil ambako ndiko kitovu cha maambukizi miili karibu 800 ilikusanywa kutoka majumbani na mitaani kwa mwezi Februari ambapo mochwari na kampuni za mazishi zilielemewa na uwingi wa maiti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...