Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MUSTAPHA Mohammed maarufu kama Mairutuwa na kiongozi maarufu wa genge la utekaji nyara nchini Nigeria ambalo pia linadaiwa kumuuwa mseminari wa Shirika la Mchungaji Mwema, Michael Nnadi (18) wa Seminari ya Mchungaji Mwema katika jimbo la Kaduna mnamo Januari 2020; ameeleza sababu ya kumuua marehemu Nnadi licha ya kukusanya fidia kutoka kwa seminari hiyo.
 
Ikumbukwe kuwa mnamo Januari 9, watu  wenye silaha walivamia Seminari hiyo na kuwateka nyara  waseminari wanne ambapo walimuua mmoja wao na kuwaachilia watatu mnamo Januari 31na hiyo ni baada ya kupata fidia kutoka kwa seminari hiyo, hata hivyo  baadaye mwili wa mseminari wanne, Michael Nnadi ulipatikana kwenye kichaka mnamo tarehe 2 Februari na kuzikwa tarehe 11 Februari mwaka huu.
 
Katika mazungumzo na gazeti la The Sun, Mustapha amesema tangu siku ambayo Nnadi alitekwa nyara, alikuwa akimuhubiria injili ya Yesu na kumwambia usoni mwake abadilishe njia zake mbaya au aangamie na kueleza kuwa marehemu Nnadi hakumruhusu kuwa na amani kila wakati alikua akihubiri Injili ya Yesu Kristo kwa ujasiri huku akijua kuwa hawako katika imani moja jambo lililopelekea kumuua Nnadi.
 
Mustapha ambaye kwa sasa yuko mahabusu akiwa washiriki wengine wawili wa genge lake, amesema kuwa waliamua kuvamia Seminari hiyo kwa sababu walijua seminari itatoa pesa nzuri na hiyo ni kwa mujibu wa habari juu ya Seminari hiyo waliyopewa na mwanachama wa genge hilo ambaye ni mfanyabiashara wa Okada (bodaboda) anayeishi karibu sana na Seminari hiyo. 

Amesema ilichukua karibu siku tano kufanya uchunguzi sahihi juu ya Seminari hiyo kabla ya kuanza operesheni hiyo.
 
Pia ameeleza jinsi walivyotumia nambari ya simu ya marehemu Nnadi kuwasiliana na viongozi wa seminari hiyo na kutaka fidia ya Naira 100 milioni ambayo baadaye ilipunguzwa hadi kufikia Naira 10 milioni iliyolipwa na viongozi wa Seminari hiyo kwa kutolewa kwa waseminari watatu.
 
Mustapha amefunguka zaidi na kueleza namna walivyowalazimisha viongozi wa shule kununua kadi za rejareja za mtandao simu na kuweka  jumla ya Naira 30,000 na kwenda nazo mahala walipokuwa wamekubaliana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...