Na Mwandishi wetu
KATIKA kuendeleza Mziki wa Dance hapa nchi Mwanamziki, Patrick Kessy ameachia kibao kipya cha "SIRI" ambacho kinafanya vizuri hivi sasa na kuwaburudisha wapenzi wa mziki hapa nchini.

Akizungumza na Michuzi blog jijini Dar es Salaam leo, Meneja wa msanii huyo wa dansi, Patrick Kessy, Abdallah Menssah, amesema kuwa wimbo wa Siri ni maalum kwa ajili ya wapenzi wa muziki mzuri na mtamu zaidi hapa nchini.

"Patrick Kessy alikuwa mdau mkubwa wa mziki wa dansi na sasa ameamua kishika mic na kuingia studio na kutoa wimbo wa 'Siri'," amesema meneja Menssah.

Katika wimbo huo, Patrick Kessy amewashirikisha waimbaji nguli wa dansi, Grayson Semsekwa aliyewahi kutamba na bendi za Extra Bongo, Twanga Pepeta na TOT, pamoja na Richard Mangustino 'Teacher'.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...