
Akihutubia wananchi leo Dodoma katika uzinduzi wa majengo ya ofisi za ikulu Chamwino, Rais Magufuli amesema watanzania wasikubali kulanguliwa mazao yao waliyozalisha kwa wingi mwaka huu.
" Nawaasa watanzania mtunze chakula na muuze kwa bei ya juu mazao mliyostawisha kwa wingi mwaka huu. Nawaambia watwange kwa bei wanunuzi. Nasema watwange," amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amesema kuanzia sasa hadi miaka miwili ijayo kutakuwa na uhaba wa chakula ktk nchi nyingi hivyo ni fursa kwa watanzania kuuzia nchi hizo chakula.Tanzania kwa mwaka huu imezalisha chakula kingi mno na nchi ina akiba ya kutosha kwa hiyo wakulima wataweza kuwauzia majirani chakula.
Nchi nyingi Afrika zilitumia ugonjwa unaosababishwa na virusi kufungia wananchi wao ndani badala ya kuwafungulia kulima hivyo watapata taabu sana kwa njaa.
Tayari wananchi wa mataifa mengine wameanza kuugua vipindipindu sababu ya kufungiwa ndani na kukosa chakula.Tumeskia juma lililopita wananchi wa Kenya 13 walivyougua kipindupindu sababu ya kufungiwa bila huduma nzuri za vyoo.
Tumeona katika vyombo vya habari Raisi wa Uganda Yoweli Museveni akiwafundisha waganda kubadili ulaji na kula tonge dogo la ugali ili kuishi.
Tumeskia nyingi na majirani zetu wanavyoangaika kupata mlo wa kushiba.
Tanzania kama nchi ya ukombozi itaziuzia nchi hizo chakula ili wananchi wake wasife na kuugua utapiamlo maana tunategemeana sana katika nyanja mbalimbali
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...