Raisi mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amempongeza sana Raisi John Magufuli kwa kufanya mambo mengi, mapya na mazuri.

Akisalimia wananchi wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi za ikulu Dodoma, mzee Mwinyi amesema Rais Magufuli anatumia fikra za ujana kufanya mambo makubwa nchini.

Baadhi ya mambo mapya na makubwa aliyofanya Raisi Magufuli ni kuhamishia serikali na wizara zote Dodoma na kujenga ikulu mpya Dodoma.

Raisi Magufuli pia anajenga mradi mkubwa wa umeme unaoitwa Mwalimu Nyerere Hydro power Project wenye zaidi ya megawati 2000 katika bonde la Rufiji.

Rais Magufuli pia amewasha umeme katika zaidi ya vijiji elfu nane tangu aingie madarakani.

Kama hiyo haitoshi Rais Magufuli yupo anajenga treni ya mwendo kasi kutoka Dar es salaam mpaka Mwanza ambapo kipande cha kwanza kutoka Dar es salaam hadi Morogoro kitazinduliwa hivi karibuni.

Yapo mengi amefanya Raisi katika kipindi cha miaka mitano angani, ardhini na majini ila nafasi haitoshi kuandika vyote hapa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...