Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
RAIS
 wa Marekani Donald Trump ameendelea kulituhumu Shirika la afya Duniani 
(WHO) kwa kushindwa kuwa chombo huru katika kupambana na janga la 
mlipuko wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona 
(Covid-19.) Ambavyo hadi sasa vimesambaa duniani kote na hakuna chanjo 
wala kinga iliyopatikana hadi sasa.
Kupitia
 barua aliyoiweka katika ukurasa wake wa mtandao wa Instagram 
akiielekeza kwa Mkurugenzi wa WHO Dkt. Tedros Adhonom Ghebreyesus Trump 
amesema, aliamua kusitisha michango ya nchi yake kwa Shirika la Afya 
Duniani( WHO) tangu Aprili 14 mwaka huu ili kufanya uchunguzi juu ya 
mambo ambayo anadai WHO ilizembea kuyafanya katika kupambana na mlipuko 
wa virusi vya Corona (Covid 19.)
Pamoja na mambo mengine mengi Trump anasema uchunguzi umebaini yafuatayo;
 WHO haijatoa taarifa kwa wakati hasa kwa kutangaza kuwa virusi vya Covid-19 kuwa janga la ulimwengu.
Pia
 ameeleza kuwa WHO imetoa taarifa za uongo na za kuaminisha dunia kwamba
 Covid -19 haiambukizwi kwa mtu na mtu licha ya baadhi ya wataalamu 
kueleza namna ya virusi hivyo vinavyosambaa.
Vilevile
 amesema kuwa WHO haikufanya utafiti wake kwa uhuru kupitia wataalamu 
wake na badala yake wakategemea taarifa za China na kuihabarisha dunia 
jambo ambalo huenda ilikuwa upotoshaji.
Aidha
 amelituhumu shirika hilo kwa kuendelea kuisifu China kwamba wanafanya 
kazi nzuri hata baada ya wao kuzuiwa kufika Wuhan kwenye kitovu cha 
ugonjwa mapema badala yake kuruhusiwa mwishoni kabisa ambapo ugonjwa 
ukiwa umeshaenea dunia nzima.
Waraka
 huo umeeleza kuwa WHO haikuwaonya China juu ya ubaguzi na unyanyasaji 
wa watu weusi  wanaoishi China  kwa madai kwamba ndio waliosababisha 
kuenea kwa Virusi vya  Corona na hiyo ni baada ya mabalozi wa nchi za 
Afrika kuandika barua kwa Serikali ya China kuhusiana na ubaguzi wa 
wananchi wa mataifa ya Afrika.
Kupitia
 waraka huo pia imeelezwa kuwa WHO iliikosoa USA kwa kuzuia wachina 
kuingia Marekani wakati huohuo ikiisifu China kwamba inalinda Dunia.
Zaidi
 sana Trump amemlaumu mkurugenzi wa WHO kwa kutoonyesha uwezo kama 
mtangulizi wake ambaye mwaka 2003 aliongoza Dunia kupambana na mlipuko 
wa homa ya Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS) ambapo aliionya 
China kuacha kutoa taarifa za kupotosha ambazo zitahatarisha usalama wa 
ulimwengu.
Hivyo Trump 
ametoa siku 30 kwa WHO kujirekebisha vinginevyo ataondoa kabisa bajeti 
yake ya kuchangia WHO na atafikiria kama kuna umuhimu wa kuendelea kuwa 
mwanachama tena kwa sababu hawezi kutumia pesa za walipa kodi wake 
kwenye mradi ambao hauna maslahi.
RAIS
 wa Marekani Donald Trump 



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...