Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
MWANDIKO
 wa mwanafunzi Prakiti Malla (16) maarufu kama "Microsoft Word" binti 
kutoka Nepal umevunja rekodi ya kuwa mwandiko bora zaidi kuwahi kutokea,
 katika mitandao mbalimbali ya kijamii hati za mwandiko wa binti huyo 
zimekuwa zikisambaa na kusifiwa kwa namna ulivyoumbwa kwa namna kuvutia 
na kusomeka kwa urahisi.
Baadhi
 ya watu wamekuwa wakitumia muda mwingi zaidi katika shule za awali 
katika kuumba herufi na stadi za uandishi na wachache hufanikiwa kuumba 
herufi kwa usahihi huku wengine wakipata wakati mgumu kwa kushindwa 
kuumba herufi na kuwa na miandiko mibovu.
Baadhi
 ya wataalamu hasa walimu wanaeleza; kuwa na stadi nzuri ya kuandika 
haina faida kwa msomaji pekee bali huvutia kwa namna ambavyo 
umepangiliwa.
Prakiti
 akiwa darasa la nane mwaka 2017 hati za mwandiko wake zilisambaa na 
kuzua mijadala katika mitandao ya kijamii hasa Twitter, mwandiko huo 
ulionekana kuwa bora zaidi kuwahi kutokea kwa mwanafunzi, herufi 
zilikuwa zimeundwa vyema na wengi wamekuwa wakifananisha mwandiko wa 
Prakiti na maandishi katika kompyuta.
Mwandiko
 wa Prakiti ulipelekea Serikali ya Nepal kuanzisha mashindano ya 
"Penmanship Competition" ambapo binti huyo aliibuka kidedea na serikali 
ikatangaza mwandiko wa Prakiti ni bora zaidi nchini humo.
Vyombo mbalimbali vya habari vilimnukuu Prakiti akieleza kuwa anatumia masaa mawili kwa siku kwa kufanya mazoezi ya kuandika.
Ni mwandiko pekee uliowafanya watumiaji wa mitandao kufikiria kuuweka mwandiko wa Prakiti katika hati za kompyuta.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...