NA MWAMVUA MWINYI,MKURANGA
 
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga na Naibu wa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amekabidhi Magodoro Sabini (70) kwa ajili ya kambi ya watu walioko kwenye karantini wilayani Mkuranga.
 
Hatua hiyo ya Ulega ni kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za serikali za kupambana na ugojwa wa Homa ya Mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona ambao umekuwa janga la Ulimwengu.
 
Magodoro hayo, Mbunge huyo aliyapokea kutoka kwa wadau na marafiki mbalimbali walioamua kuunga mkono jitihada za serikali kupambana dhidi ya corona.
 
Akipokea magodoro hayo ,mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga alimshukuru Mbunge Ulega kwa jitihada hizo na amewaomba wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi hizi za serikali za kupambana dhidi ya corona.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...