MASUPASTAA kibao wa Bongo Dansi hivi sasa wamekimbilia jijini Arusha katika kitongoji cha Munduli walipoanzisha bendi ya Wisdom Music Band inayofanya vizuri hivi sasa.
Akizungumza na mwandishi wetu jijini Dar es Salaam, bosi wa bendi hiyo, Nyuchi amesema kuwa, alishawishika kuanzisha kundi hilo baada ya wasanii wengi kumfuata kutaka msaada wake kisanii.
"Nimeanzisha kundi hilo ambalo linakusanya wanamuziki wengi mahiri, ili kusapoti jitihada za kuinua muziki wetu wa Dansi, hivyo naamini kundi hili litakuwa poa muda si muda," amesema Boss huyo.
Baadhi ya mastaa wanaopatikana kwenye bendi hiyo ni pamoja na Rama Igwe, Jua Kali, Awadh Muhumba, Sele Muhumba, Komba Bass, Cath Cindy, Elias Ngoma na Awadh Muhumba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...