Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
ANAFAHAMIKA
kwa jina la Edward Saidi 'Tingatinga' mchoraji wa kitanzania ambaye pia
anaelezwa kuwa ni mwanzilishi wa mtindo wa uchoraji maarufu kama
Tingatinga, ambao umekuwa kivutio kwa watalii na umekuwa ukifanywa
katika nchi za Tanzania, Kenya na baadhi ya maeneo katika ukanda wa
Afrika Mashariki.
Tingatinga
ni sanaa ya ufundi inayojumuisha uchoraji, upakaji rangi, ufinyanzi,
uchongaji na utengenezaji wa mapambo ya asili na utamaduni.
Tingatinga
alizaliwa mwaka 1932 katika kijiji cha Namocheli, Mindu karibu na
kijiji cha Nakapanya mkoani Tunduru, Kusini mwa Tanzania karibu na mpaka
wa nchi ya Msumbiji.
Alifahamu hakukuwa na wajuuzi wa kazi hiyo katika eneo alilokuwa akiishi akaamua kujitosa na kuifanya na aliifurahia.
Ndugu
wa Tingatinga bado wanaishi, upande wa mama yake wanaishi katika vijiji
vya Nakapanya, Mindu na Mtonya na ndugu wa baba zake wanaishi Ngapa
kilomita 20 kutoka Kaskazini mwa Nakapanya.
Edward
Tingatinga alizaliwa kwenye familia ya kimaskini, mama yake alikuwa
Agnes Binti Ntembo kabila la mmakua na baba yake Saidi Tingatinga
aliyekuwa Mngindo na Tingatinga alipewa majina ya dini zote kutokana na
mfumo wa matrilinia unaofuatwa na kabila la wamakua, Tingatinga
alilelewa zaidi na upande wa mama na hiyo ni baada ya mahusiano ya
wazazi wake kuvunjika.
Mwaka
1950 Edward alimwacha mama yake na kwenda kufanya kazi katika mashamba
ya mkonge Mkoani Tanga, baadaye akaalikwa kwenda Dar es Salaam na mjomba
wake Salum Mussa Mkaoya aliyekuwa anafanya kazi ya upishi kwa ofisa ya
kiingereza, na alipofika akaajiriwa kama mtunza bustani.
Wakati
huohuo alianza kujifunza Muziki na mwaka 1968 uchoraji, alichora kwa
kutumia malighafi za bei rahisi ikiwemo rangi ya kung'arisha baiskeli
na mabaki ya vigae na malighafi za ujenzi.
Michoro
yake ilikua halisi na inayoakisi maeneo ya Afrika hasa Tanzania na hasa
alichora wanyamapori na maeneo ya vivutio yanayopatikana Tanzania.
Mwaka
1970 alimuoa Agatha Mataka mmakonde kutoka Msumbiji na wakati huo
michoro yake ya Tingatinga ilikua inafahamika sana kwa wakazi wa Ulaya
nchini Tanzania na watalii hapo ndipo akaanza kutumia muda wake wote
katika sanaa hiyo.
Baadaye
akaanzisha kundi 'Tingatinga Art Co-operative Society' na moja wa
wanakikundi hao ni pamoja na January Linda, Adeus Mandu, Ajaba
AbdallahMtalia, Casper Tedo, Simon Mptata na Omari Amonde hilo ndilo
lilikuwa kundi la kwanza la wanafunzi waliojifunza sanaa ya Tingatinga,
na kati yao Omari Amonde ambaye ni mpwa wa Omari ndiye anayeishi.
Maisha
ya Edward Saidi Tingatinga yalikatishwa mwaka 1972 kwa bahati mbaya,
polisi walimfyatulia risasi kwa kudhani kuwa ni mhalifu na alizikwa
katika makaburi ya Msasani Dar es Salaam.
Shule
za Tingatinga bado zinaishi na zimekua na kufanyiwa marekebisho kwa
kiasi kikubwa na kuwa na wafuasi wengi na vivutio kwa watalii katika
nchi za Tanzania, Kenya na sehemu kubwa ya Mashariki mwa Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...