Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo akizindua eneo la kunawa mikono katika kukabiliana na maambukizi ya Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona (COVID-19) katika shule ya sekondari ya Tumaini, mkoani Singida ambapo wanafunzi zaidi ya 100 wanajiandaa kwa mtihani wa kidato cha Sita. Kulia kwake anayeshuhudia ni Mkuu wa wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula.
Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo akiongea na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Tumaini wanaojiandaa na mtihani wa kidato cha Sita ambao amewakabidhi vitakasamikono ambavyo kila mmoja ataweza kutumia kwa muda wa siku 60. Aidha, jumuiya ya shule hiyo pia ameikabidhi miundombinu ya kunawa mikono
Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo (kushoto) akimkabidhi mmoja wa wafanyakazi wa shule ya sekondari ya Tumaini vitakasamikono kwa niaba ya jumuiya ya shule hiyo katika hafla  fupi ya kukabidhi miundombinu ya kunawa mikono na vitakasamikono iliyofanyika shuleni hapo.
Sehemu ya vitakasamikono ambavyo wanafunzi wa shule ya sekondari ya Tumaini, mkoani Singida wamekabidhiwa . Vitakasamikono hivyo vimeandaliwa Idara ya Ubora wa Maji, Wizara ya Maji, ni moja ya mchango wa sekta ya maji katika mapambano dhidi ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...