Mkuu wa kitengo cha Ustawi wa Jamii na Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Salum akimkabidhi Mr. Jackson Msilambo Tsh. 4,370,000/= zilizotolewa na Mchungaji Rose Shaboka kutoka kanisa la New Day Church kwa ajili ya gharama za matibabu ya mtoto wake anayetibiwa JKCI leo Jijini Dar es Salaam.
 Baba wa mtoto anayetibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mr. Jackson Msilambo akimpa mkono wa shukrani Mchungaji Rose Shaboka kutoka kanisa la New Day Church baada ya kukabidhiwa Tsh. 4,370,000 kwa ajili ya gharama za matibabu ya mtoto wake anayetibiwa JKCI leo Jijini Dar es Salaam
Mchungaji wa kanisa la New Day Church Rose Shaboka akimjulia hali mtoto wa Jackson Msilambo baada ya kuchangia gharama za matibabu ya mtoto huyo anayetibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo Jijini Dar es Salaam. Pia Mchungaji Rose amechangia kiasi cha Tsh. 500,000/= kama gharama za matibabu pamoja na gharama za kupatiwa bima ya afya kwa mtoto mwingine anayetibiwa JKCI.
Picha na: JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...