Mchumi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri
Mkuu, Bi. Sarah Mshui akieleza jambo kuhusu masuala ya Hifadhi ya Jamii
kwa wadau walipokutana kwa ajili ya mafunzo maalumu ya kujengewa uelewa
kuhusu Kinga ya Jamii katika Ukumbi wa Mikutano wa PSSSF, Jijini
Dodoma.
Sehemu ya wadau wakijadili jambo wakati wa mafunzo hayo ya kuwajengea uelewa kuhusu masuala hifadhi ya jamii.
Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka
TAMISEMI, Bi. Mariam Nkumbwa (kushoto) akichangia mada wakati wa mkutano
huo uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa PSSSF, Jijini Dodoma.
Mtaalamu wa Kinga ya Jamii, Dkt. Flora Miyamba akitoa mada kwa wadau kuhusu masuala ya Kinga ya Jamii.
Afisa Maendeleo ya Jamii, kutoka
Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bi. Herieth
Mwamba (kushoto) akieleza jambo wakati wa mkutano huo.
Baadhi ya wadau
waliohudhuria mafunzo hayo wakiwa wamewaka daftari “Notebook” kichwani
kama ishara ya kumkinga wananchi na changamoto mbalimbali. PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU
(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
OWM – KVAU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...