WAZIRI wa Maji wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa amerejesha fomu ya kuwania uteuzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mgombea wake wa urais Zanzibar.

Profesa Mbarawa alichukua fomu Juni 19,  mwaka huu katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui mjini Unguja, akiwa mwanachama wa 10 kufanya hivyo.

Hivyi leo Juni 27,2020  amerejesha fomu hizo katika ofisi hiyo na kupokewa na Katibu wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar, Galous Nyimbo.

Wakati alipochukua fomu hiyo Profesa Mbarawa aliwaambia waandishi wa habari kuwa amemtanguliza Mwenyezi Mungu katika safari hiyo na kuwataka wamuombe jambo alilolianzisha likawe na baraka kwake.

Hata hivyo baada ya kurejesha fomu leo amekishukuru Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kusimamia vizuri mchakato huo wa kuwania uteuzi wa kugombea urais wa Zanzibar.

Mbali ya kuwa Waziri wa Maji, Profesa Mbarawa amewahi kuhudumu katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika Serikali ya Rais John Magufuli.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...