Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM NEC mara baada ya kuanza kwa Kikao ambacho kilikuwa na ajenda mbalimbali ikiwemo ya Uchaguzi wa Mgombea wa Urais kwa upande wa Zanzibari ambapo Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi alichaguliwa kuwa kuwa Mgombe Urais kwa Tiketi ya CCM kwa upande wa Zanzibar leo tarehe 10 Julai 2020 katika Ukumbi wa White House jijini Dodoma
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM NEC kilichofanyika katika ukumbi wa White House jijini Dodoma leo tarehe 10 Julai 2020.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM-Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein, Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula mara baada ya kuanza kikao cha NEC katika Makao Makuu ya CCM White House jijini Dodoma
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi katika Mkutano huo wa NEC uliofanyika katika Makao Makuu ya CCM White House jijini Dodoma. PICHA NA IKULU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...