NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
KATIKA
Kura za maoni mkoani Pwani ,Upande wa UWT ,ubunge viti maalum ,Subira
Mgalu ameshinda kwa kura 252 dhidi ya wagombea wenzake 26 waliojitokeza
kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo .
Katika kinyang'anyiro hicho ,Hawa Mchafu na Zainab Vullu wamepata kura 227 ambapo wameshika nafasi ya pili .
Kinyang'anyiro
hicho kilichoanzia asubuhi na kumalizika saa 9.30 alfajili ya Julai 24
ukumbi wa Filbert Bayi mjini Kibaha, chini ya usimamizi wa Aboubakary
Kunenge Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akisaidiwa na Lukhia Masenga
Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Bagamoyo na Anastazia Amas Katibu wa CCM
Mkoa wa Pwani.
Katika
kinyang'anyiro hicho Mgalu alijinyakulia kura 252, Hawa Mchafu kura 227,
Zaynab Vulu 227, Nancy Mutalemwa 102 huku Mwenyekiti wa UWT Mkoa Farida
Mgomi akipata kura 58, huku wagombea wa nafasi zingine waliopigiwa kura
katika nafasi zao walizoziomba.
Akitangaza
matokeo Kunenge aliwataja washindi na nafasi zao ziko kwenye mabano
kuwa ni Tabia Kalega (Wasomi 203), Zaynabu Gama (Taasisi Binafsi 312),
Blandina Sengu (Walemavu 180),
Dr. Halisi Kaijage (Wafanyakazi 160) .
"Nasisitiza
kwamba washindi ambao tumewapata hapa ni hatua ya awali, majina yao
yatapelekwa ngazi nyingine jijini Dodoma ambako huko kutakuwa na zoezi
lingine linalofanana na hili "
Anastazia
aliwataka viongozi wa chama hicho na Jumuiya kufuata utaratibu
uliotumika kwenye uchaguzi huo katika uchaguzi wa Madiwani wa Kata na wa
Viti Maalumu kwa lengo la kuepukana na malalamiko kutoka kwa washiriki.
Zoezi
hilo lilikuwa na wagombea 43 katika nafasi za Ubunge wa Viti Maalumu
uliogawanyika makundi matano ambayo ni la Wafanyakazi, Walemavu, Ngo's,
Wasomi na Viti Maalum nafasi tatu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...