NA MWAMVUA MWINYI,PWANI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM )mkoani Pwani kimewaasa baadhi ya wanachama wake kuondoa makundi na kuacha kuwekeana chuki badala yake waungane kuwa wamoja na kushikana baada ya uchaguzi wa ndani kukamilika .

Kimeeleza ,kwasasa hatua mbalimbali zitaendelea na vikao vya maamuzi ya kuteua wagombea watakaopeperusha bendera katika uchaguzi mkuu unaokuja hivyo haina budi kuwa watulivu na upendo .

Akielezea mchakato wa uchaguzi walivyojipanga baada ya hatua za awali za chama kukamilika ,katibu wa CCM mkoani Pwani ,Anastazia Amas alisema mkoa umejidhatiti kushinda kwa kishindo chaguzi nafasi ya Urais,wabunge na madiwani.

Alieleza ,haina ubishi mchakato wa kura za maoni umeenda kidemokrasi hivyo kilichobakia sasa ni kuwa wamoja .

"Chuki na visasi kwasasa havina nafasi ,wanachama wawe pamoja ,sio kama wapo wanaowekea chuki bali  katika uchaguzi wowote hakukosekana makundi lakini sasa vitendo hivyo vifikie kikomo:"alielezea Amas .

Amas alifafanua, hatua za uchukuaji wa fomu ulikuwa wa kidemokrasia ,wanachama walijitokeza kwa wingi kuanzia ubunge wa majimbo Tisa na ubunge viti maalum,madiwani.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...