Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

Uongozi wa Klabu ya Dodoma Jiji umeweka wazi kikosi cha wachezaji 26 kitakachoshiriki Ligi kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2020/21.

Dodoma Jiji, imewatangaza wachezaji hao leo hii na kuwajulisha mashabiki wake kuwa kikosi chao kimekamilisha usajili wake kwa ajili ya kuimarisha timu hiyo kuelekea msimu ujao.

Wachezaji waliotangazwa kuwepo katika kikosi hicho ni pamoja na magolikipa watatu  Hussein Masalanga, Emmanuel Mseja na Aron Kalambo.

Wengine ni mabeki, Anderson Solomon, Abubakari Ngalema, Ibrahim Ngecha, Mbwana Kibacha, Hassan Kapona, George Wawa, Jukumu Kibanda, Augustino Ngata na Justine Omary.

Kwa upande wa Viungo ni  Rajab Seif, Steven Mganga, Jamal Mtegeta, Omar Kanyoro, Deus Kigawa, Salmin Hoza, Cleophace Mkandala, Peter Mapunda na Dickson Ambundo.

Washambuliaji  Anuary Jabir, Khamis  Mcha, Santos  Thomas, Seif Karihe na Michael Chinedu.

Timu iyo kwa sasa ipo katika maandalizi ya msimu mpya unaoatarajia kuanza Septemba 06  baada ya kupanda ligi kuu msimu wa 2020/21

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...