Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi amewapongeza TFS shamba la miti la Sao Hill kwa kujenga la bweni la shule ya sekondari ya Changalawe kwa kutumia zaidi ya milioni 114 iliyopo Mafinga Mjini katika wilayani ya mufindi .
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa na mkuu wa shule ya sekondari ya Changarawe wakati wa kukagua ujenzi wa bweni lilofadhiliwa na Sao Hill
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa na mkuu wa shule ya sekondari ya Changarawe wakati wa kukagua ujenzi wa bweni lilofadhiliwa na Sao Hill


NA FREDY MGUNDA,MUFINDI.
 
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi amewapongeza TFS shamba la miti la Sao Hill kwa  kujenga la bweni la shule ya sekondari ya Changalawe kwa kutumia zaidi ya milioni 114 iliyopo Mafinga Mjini katika wilayani ya mufindi na kuwaomba wadau wengi wajitolee kama ambavyo Sao hill walivyofanya

Hayo yamesemwa mara baada ya ukaguzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari Changalawe wilayan Mufindi lililojengwa na Wakala wa misitu Tanzania TFS kupitia shamba la miti Sao hill lililogharibu zaidi ya sh. Milioni 114.

Akizungumza na wafanyakazi na wanafunzi wa shule hiyo,Hapi alisema kuwa jingo la bweni alilololikagua ameridhika nalo kutokana na thamani ya fedha kutumika kikamilifu kwa kuzingatia ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wadau wa serikali ndio maana jingo hilo limejengwa kwa viwango stahili.

Hapi aliwataka walimu kuendelea kutoa elimu bora kwa wanafunzi wa shule hiyo ili kuzalisha kizazi cha wasomi wenye maarifa  ya darasani na maisha kwa ujumla kwa kuwa shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri  kiwilaya,mkoa na taifa kwa ujumla.

Katika risala ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga Saada Mwaruka iliyosomwa na mkuu wa shule ya Sekondari  Changarawe imebainisha kuwa ufadhiri huo utasaidia jumla ya wanafunzi 80 kukaa shuleni hapo na kuondokana na hatari ya kukatisha masomo kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo tatizo la mimba kwa wanafunzi.

Alieleza namna Jitihada zake za kuandika miradi ya utatuzi wa changamoto za shule ulivyosaidia kuwavutia wafadhiri hao ambao Sao Hill hadi kufanikisha upatikanaji wa majengo kadhaa ikiwemo bweni hilo.

Hatua hii imeonesha kumpendeza mkuu wa Mkoa Ally hapi licha ya kuwataka viongozi wengine wa taasisi za serikali ikiwemo shule kujenga utamaduni wa kuandika miradi yenye kuomba ufadhiri kwa wadau ametoa maagizo kwa wakuu wa wilaya zinazokutikana wilani huo

 Kando ya hayo awali katika ziara hiyo mkuu wa mkoa amefanya uzinduzi wa jengo la maabara katika zahanati ya Rungemba wilayani humo...na kuahidi kukabidhi mifuko 100 ya saruji ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za wananchi hao waliojitoa kuchangia na kukamilisha ujenzi wa maabara hiyo.

Maeneo mengine yalifikiwa na mkuu wa mkoa katika ziara hiyo iliyobatizwa jina la Iringa mpya ni pamoja na hospitali ya halmashauri ya Mji wa Mafinga pamoja na eneo la ofisi za shamba la miti sao hill ambapo amepokea mtambo wa kisasa wa kuzimia moto ulionunuliwa na Serikali na kisha .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...