Na Denis Mlowe, Iringa
TAMASHA kubwa lijakulikana kwa jina la Iringa  All Stars linatarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Klabu VIP na kuwakutanisha mastaa mbalimbali wanaoishi mkoani Iringa.

Tamasha hilo  linaloandaliwa na mkurugenzi wa kampuni ya Iringa Finest Ramadhan Shemhilu lina lengo la kutengeneza kipato kwa wasanii wanaoishi mkoani hapa kujikomboa kiuchumi.

Akizungumza na mwanahabari hizi, Shemhilu alisema kuwa licha ya kuwaongezea kipato wasanii lina lengo pia kuwakutanisha mashabiki zao ambao wamekuwa wakiwasikia katika vyombo mbalimbali vya habari mkoani hapa.

Alisema kuwa tamasha hilo ni la kujivunia cha kwa wasanii mbalimbali ambapo kutakuwa na tasnia mbalimbali za burudani ikiwemo sanaa ya uchekeshaji.

"Licha bongo fleva kutakuwa na burudani mbalimbali kama Maonyesho ya mavazi na live band kutoka bendi za  Iringa." Alisema

Aliongeza kuwa tamasha hilo litakuwa mahususi kwa wasanii na vijana mbalimbali kuonyesha vipaji vyao ambao Kuna wadau mbalimbali wameahidi kuwasaidia vijana hao.

Alisema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika kikubwa ni watu kujitokeza kwa wingi kushuhudia vipaji mbalimbali ikiwemo wasanii wa bongo movie mkoani hapa kuonyesha kazi zao.

Aidha alisema kuwa mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mgombea ubunge Iringa Mjini kwa tiketi ya CCM Jesca Msambatavangu na litaanza kuanzia saa moja usiku.

Mratibu wa tamasha la Iringa All Stars mkurugenzi wa kampuni ya Iringa Finest Ramadhan Shemhilu.

Baadhi ya wasanii wakiwa kwenye mazoezi ya tamasha hilo.
(Picha zote na Denis Mlowe)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...