Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa akisisitiza
jambo wakati alipotembelea banda la TRA katika viwanja vya Nyakabindi,
Mkoani Simiyu. Wakwanza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka.
Wazee wakipatiwa elimu kuhusu msamaha wa kodi ya majengo kwa wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60
Delina Lema, Afisa Msimamizi wa Kodi akimkabidhi mfanyabiashara cheti cha Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) baada ya kumsajili
Anthony Faustin Afisa, Msimamizi wa Kodi, akitoa elimu wakati wa maonesho ya Naenane
Afisa Msimamzi wa Kodi wa TRA, Delina Lema (kulia) akimkabidhi
mwananchi leseni ya udereva wakati wa maonesho ya Nanenane yanayoendelea
katika Viwanja vya Nyakabidi Simiyu.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa (kushoto) na
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka (kulia) wakimkisikiliza Afisa
Msimamizi wa Kodi Lameck Ndinda akitoa maelezo kuusu huduma ambazo TRA
inazitoa kwa wananchi wanaotembelea banda la TRA.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent
Bashungwa ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuendelea kukusanya
mapato ya serikali kwa ufanisi mkubwa.
Mheshimiwa Bashungwa ametoa pongezi hizo
alipotembelea banda la (TRA) kujionea shughuli na huduma ambazo TRA inazifanya
katika Maonesho ya Nanenane ambayo yanafanyika Kitaifa katika viwanja vya
Nyakabindi, Mkoani Simiyu.
“Nawapongeza sana TRA mnafanya kazi nzuri sana ya kukusanya mapato na mnashirikiana vizuri na Wizara ya Viwanda na Biashara”, alisema Mhe. Bashungwa.
Pamoja na pongezi hizo, Waziri Bashungwa
ameitaka TRA kuwasimamia vizuri wasambazaji wa mashine za kielektroni za kodi (EFD)
kwa kuondoa kero ya kufutika kwa karatasi za mashine za hizo.
Aidha ameishauri TRA kuendelea kuweka mazingira mazuri na wezeshi kufanya biashara ili mapato ya nchi yaongezeke.
Aidha ameishauri TRA kuendelea kuweka mazingira mazuri na wezeshi kufanya biashara ili mapato ya nchi yaongezeke.
Mamlaka ya Mapato Tanzania ikiwa ni miongoni
mwa taasisi za serikali zinazoshiriki maonesho ya Nanene inatoa elimu na huduma
mbalimbali katika viwanja vya maoenesho ambapo kati ya huduma zinazotolewa ni pamoja
na kutoa leseni za udereva kwa waombaji wapya na wale
ambao leseni zimeisha muda wake huduma ambayo imekuwa kivutio kwa washiriki wa
maonesho.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti baada ya kupokea leseni zao za udereva, baadhi ya wenye
leseni wameipongeza TRA kwa uamuzi wa kutoa huduma hiyo ambayo inapatikana kwa
urahisi na haraka.
“Sikutegemea
kama nitapata leseni yangu haraka namna hii. Kwa kweli nawapongeza sana”,
amesema Rayner Nicholause ambaye ni mkazi wa Dodoma.
Naye
Andes Seiya mkazi wa Arusha amesema kwamba huduma ni nzuri kwani amepata leseni
yake ndani ya siku moja baada ya kulipia. “Tunaomba huduma hii iboreshwe huko
mikoani kwani kama imewezekana hapa katika maonyesho kwanini cihukue muda mrefu
kupata leseni ya udereva katika ofisi za TRA?” alisema Seiya.
Kwa
upande wake Nelson Mnyanyi ambaye ni Mkazi wa Dar es Salaam amesifu utoaji wa
huduma katika banda la TRA na kusema kwamba ni huduma bora na zinatolewa haraka na hivyo kuokoa muda. “Baada ya kupata
taarifa kwamba leseni yangu ipo tayari nifike niichukue baada ya kulipia
sikuamini. Nawashukuru na nawapongeza sana”, alisema Mnyanyi.
Mbali
na kutoa leseni za udereva, huduma nyingine ambazo TRA inazitoa katika maonesho
ya Nanenane ni pamoja na kutoa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) kwa
wafanyabiashara na watu binafsi, kutoa ankara za Kodi ya Majengo, kutoa elimu
ya kodi katika shughuli za kilimo na elimu ya kodi kwa ujumla.
Aidha
huduma nyingine ni kutoa maelezo ya fursa za masomo ambazo zinapatikana katika
Chuo cha Kodi (ITA) ambacho kinamilikwa na TRA pamoja na namna ya kutuma maombi
katika chuo hicho.
Maonesho
ya Nanenane yenye kauli mbiu, ‘Kwa Maendeleo ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi Chagua
Viongozi Bora’, yanafanyika katika viwanja vya Nyakabindi Wilaya ya Bariadi
katika Mkoa wa Simiyu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...