WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amefaya ziara ya kutembelea mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita unaotekelezwa na TBA kama Mkandarasi na Mshauri Elekezi. Akiwa katika eneo hilo la Mradi amefurahishwa na kasi ya ujenzi huo na kuipongeza TBA kwa kuendelea kutekeleza mradi huo katika ubora wa hali ya juu.

Pia Waziri Ummy amemshukuru sana Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo na miradi mingine ya Afya kote Nchini.

Vile vile kipekee ameipongeza TBA kwa kuendelea kutekeleza miradi katika kiwango cha juu. Aliongeza pia kwa kumpongeza Meneja wa TBA Mkoa wa Geita Mhandisi Gladys Jefta kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ujenzi unakwenda vizuri.

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Eng. Robert G. Luhumbi ameipongeza TBA kwa kazi nzuri iliyofanyika katika ujenzi wa hospitali hiyo huku akimpongeza meneja wa TBA na wasaidizi wake. Vile vile Mhe. Mkuu wa Mkoa ameshukuru Mhe. Rais. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuleta mradi huo wa hospitali kwani utasaidia kuokoa maisha ya wanawake wengi wakati wa kujifungua pamoja na wagonjwa wengine watakaopata huduma katika hospitali hiyo ya Rufaa. 

Meneja wa TBA Mkoa wa Geita Mhandisi Gladys Jefta amemshukuru Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwa kutembelea mradi ya Afya ambao unatekelezwa na TBA kwa mfumo wa buni - jenga (Design & Build). Aliongeza pia kuwa amefarijika sana kuona Waziri ametambua kazi inayofanywa na TBA kuwa ni yenye ubora na ameahidi kuyafanyia kazi yale yote ambayo Waziri ameagiza.

Aidha Mhandisi Gladys amempongeza Mhe. Rais. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwekeza kwenye Sekta ya Afya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...