Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imeandaa kongamano litakalowakutanisha wataalam hao lengo ni kujadili jinsi gani ya kufikia ubora ili kuongeza thamani katika Sekta ya ununuzi na ugavi kutokana na chamgamoto mbalimbali za Ununuzi na Ugavi katika Sekta za Umma na Binafsi.
Akizungumza
Jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi Matendaji wa bodi hiyo, Godfred
Mbanyi amesema kongamano hilo litawakutanisha wadau zaidi ya 1000
kutoka Ndani na nje ya Nchi ili kupeana uzoefu kutokana na sekta hiyo
kuwa nyeti katika kuongeza pato la Taifa ikiwa ni pamoja na utekelezaji
wa miradi mbalimbali ya Serikali.
Mbanyi
amesema katika Kongamano hilo Wataalamu hao watapata nafasi ya
kujadili, kuchambua, kuweka mikakati ya uboreshaji katika Sekta ya
Ununuzi na Ugavi katika Ununuzi wa Umma na Kampuni Binafsi.
"Michakato
ya Ununuzi na Ugavi katika Sekta ya Umma maana take tunatoa huduma
nzuri kwa Wananchi, pia mchakato huo unapoenda vizuri basi Serikali
inapata Kodi", amesema Mbanyi.
Amesema
Sekta ya ununuzi na ugavi inaposimamiwa vizuri inasaidia Serikali
kupata mapato yake hivyo kongamano hilo litasaidia wadau hao kutoa fursa
kwa wafanyabiashara pamoja na Makampuni kutangaza Biashara zao.
Kongamano
hilo ni la 11 ambalo linatarajiwa kufanyika Jijini Arusha Disemba 2
hadi 5mwaka huu, huku miongoni mwa Nchi zinazotarajiwa kushiriki ni
pamoja na Nchi ya Kenya, Rwanda, Burundi pamoja na Uganda.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB)
Godfred Mbanyi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uandaaji wa kongamano
litakalowakutanisha Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi lengo ikiwa ni
kujadili jinsi gani ya kufikia ubora ili kuongeza thamani katika Sekta
hiyo. Kongamano hilo ni la 11 linatarajiwa kufanyika Jijini Arusha
Disemba 2 hadi 5 mwaka 2020.
Baadhi ya wajumbe wa kongamano litakalowakutanisha Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB Godfred Mbanyi alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Kongamono hilo litakalofanyika mkoani Arusha.

Baadhi ya wajumbe wa kongamano litakalowakutanisha Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB Godfred Mbanyi alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Kongamono hilo litakalofanyika mkoani Arusha.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Godfred Mbanyi (katikati waliokaa)
akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa watakaosimamia
maandalizi ya Kongamano hilo mara baada ya kumaliza kuongea na waandishi
wa habari leo katika ofisi za PSPTB jijini Dar es Salaam


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...