Mshambuliaji wa zamani wa Barcelona Luis Suarez.
Na Agness Francis, Michuzi tv
MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa Luis Suarez mwenye uraia wa Uruguay ambaye alikuwa akikipiga katika timu ya Barcelona nchini Spain, Ametuhumiwa na chombo cha uhamiajj nchini Italia kwa kufanya udanganyifu wa kuingia kufanya mtihani wa uraia akiwa na majibu ya mtihani huo.
Kwa mujibu wa sky Itali imeripoti kuwa Suarez alikuwa katika mpango wa kupata uhamisho wa kujiunga na kikosi cha timu ya Juventus nchini humo.
Ambapo mchezaji huyo ilibidi kufanya kwanza mtihani wa kawaida ili kujua uwezo wake wa kutumia lugha za kiitaliano ili aweze kukizi kigezo cha kupewa pasipoti ya Itali.
Hivyo basi kulingana na uchunguzi wa awali imebainika kuwa maswali yalikuwa katika mtihani tayari Suarez alikuwa amepita mapema, Na hapo ndipo alipotiliwa shaka kwani hawezi kuongea neno lolote la kiitaliano.
Aidha upande wa kikosi cha Juventus wao tayari wameshakamilisha nafasi za wachezaji wa kigeni ambao hawatoki katika mataifa ya umoja wa ulaya kwa msimu huu, Na Suarez wangeweza kumsajili tu endapo angepata uraia wa Itali
Kwa mujibu wa ripoti ya pande zote mbili zilikuwa zinadai kuwa tayari wamekamilisha makubaliano binafsi, Lakini dili holo limegonga mwamba kwa sababu ya uraia
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...