Na Agness Francis, Michuzi Tv
BAADA ya kula kichapo cha mabao 4-0 dhidi ya KMC FC ikiwa ulikuwa ni mchezo wa kwanza ligi kuu Vodacom Tanzania bara, kikosi cha Mbeya Fc leo asubui kimefanya mazoezi kujinoa kwa ajili mchezo wao unaofuata dhidi ya Yanga.
Yameelezwa hayo katika ukurasa wa Instagram wa timu hiyo ya Mbeya city iliyokita maskani yake Jijini Mbeya.
Katika mtandao wa kijamii wa Mbeya City umesema kuwa "Kikosi chetu kimefanya mazoezi leo asubuhi kwa ajili ya maandalizi ya kuelekea mchezo wetu unaofuata dhidi ya Yanga."
Mchezo huo wa pili utachezwa septemba 13 katika uwanja wa Mkapa Jijini Dar es Salaam majira ya saa moja jioni dhidi ya wenyeji wao vijana wa jangwani Yanga SC.
Ambapo timu ya Yanga walilazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya wajela jela Tanzania Prison katika mchezo wa raundi ya kwanza uliopigwa katika uwanja Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kikosi hicho cha Mbeya City kina kibarua kizito dhidi ya Yanga kutafuta alama tatu ili kujiweka katika nafasi nzuri kwa kupata matokeo mazuri ikiwa ni mwanzo wa ligi ili kukwepa adhaa ya kucheza play of kama msimu uliopita 2019-20.
Vijana hao wa Mbeya City ambapo walinusurika kushuka daraja ikiwa nafasi ya 15 na kujikusanyia alama 45 kibindoni na kulazimika kucheza play of dhidi ya Geita Sc iliopo dalaja la kwanza kwa kuanzia ugenini ambapo walilazimishwa sare ya kufungana bao 1-1
Katika mchezo wa marudiano Mbeya city waliwakaribisha Geita Sc katika dimba la uwanja wa Sokoine na Mbeya city kuibuka washindi kwa bao 1-0 kupitia kwa beki wa Geita kujifunga kwa kupiga kichwa cross ya mchezaji wa Mbeya City Peter Mapunda,
Goli hilo lilidumu mapaka dakika 90 za mchezo kumalizika na kuinusuru timu ya Mbeya City kusalia kubaki katika ligi kuu vodacom Tanzania bara.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...