SERIKALI
imetumia zaidi ya sh. bilioni 6.318 kwa ajili ya ujenzi wa miradi kwenye vijiji
mbalimbali vya wilaya ya Mkalama, mkoani Singida ili kuwaondolea adha ya maji safi
wananchi wake.
Hayo yamesemwa
jana (Jumanne, Septemba 15, 2020) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati
akizungumza na wananchi waliohudhuria mkutano wa kuwanadi wagombea ubunge na
udiwani wa CCM uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya mabasi Gumanga, wilayani
Mkalama.
Mheshimiwa
Majaliwa ambaye alikuwa mkoani Singida kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi
ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, alisema Serikali ya awamu ya tano imejenga miradi
ya kimkakati zaidi ya 1,490 kwenye sekta ya maji nchi nzima.
Akifafanua
baadhi ya miradi iliyofanyika katika kipindi cha mwaka 2015/2016
na 2019/2020, Mheshimiwa Majaliwa alisema kati ya fedha hizo, sh. bilioni 1.37 zimetumika
kwa ajii ya mradi wa maji vijiji vya Mughano, Ngimu, Mgori, Malolo, Kijota, Ghaluyangu
na Mangida.
“Miradi mingine ni mradi wa maji kijiji cha Mwankoko ‘B’ ambao umetumia
shilingi milioni 656, na mradi wa maji kijiji cha Kisaki ambao umetumia shilingi
milioni 551. Pia, shilingi milioni 428 zimetumika kwa ajili ya mradi wa
usambazaji wa maji kijiji cha Gumanga na shilingi milioni 910 zimetumika kwa
ajili ya mradi wa usambazaji wa maji kijiji cha Nyahaa,” alisema.
Akifafanua zaidi, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. milioni 341 zimetumika kwa
ajili ya mradi wa uchimbaji wa visima virefu saba katika maeneo ya Nduguti, Kisuluiga,
Matongo, Ipuli, Mkiko, Mwanga, Wangeza, Kinampundu, Kinyangiri, Msingi, Senene,
Milade, Mbigigi, Nduguti (visima viwili), Tumuli (kisima kimoja) na Ibaga (kisima
kimoja).
Alisema sh. milioni 158 zimetumika kwa ajili ya mradi wa uboreshaji maji katika
kijiji cha Nduguti na sh. milioni 70 zimetumika kwa ajili ya uboreshaji maji katika
kijiji cha Kinyangiri.
Mbali ya juhudi zote hizo, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. bilioni 1.37 zimetumika
kwenye mradi wa maji kwa vijiji 10 vya Ibaga, Lyelembo, Mpambala, Ikolo, Kinyambuli,
Ipuli, Makuro, Donimic, Ishinsi Nkalalala na Lukomo.
Wakati
huohuo, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. milioni 235.98 zimetumika kwa ajili ya uchimbaji wa visima visima virefu na vifupi 20 ikiwa ni pamoja na ufungaji wa pampu za mkono.
Alisema
kiasi kingine cha sh. milioni 144 kimetumika
kwa ajili ya upanuzi wa mradi wa maji kijiji cha Mntamba na sh. milioni 85 nyingine
zimetumika kwa ajili ya ukarabati wa mradi wa maji kijiji cha Ipuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...