Hivyo yeyote ambaye atabainika kuingiza bidhaa ambazo hazijakidhi ubora atachukuliwa hatua za kisheria.
Ameyasema hayo leo Mkaguzi Mwandamizi kutoka Shirika la Viwango Tanzania TBS, Mhandisi Donald Manyama baada ya Shirika hilo kufanya ukaguzi katika Supermarket kadhaa Jijini Dar es Salaam na kubaini baadhi ya bidhaa kutokidhi viwango.
Akizungumza baada zoezi hilo kumalizika Mhandisi Manyama amesema wamefanya ukaguzi na kubaini bidhaa hizo hazina muda wa kuzalishwa (Production date) na muda wa mwisho wa matumizi (Expire date).
"Bidhaa
ambazo tumezibaini kuwa na makosa ni Shower gel,Shampoo,Conditioner na
Hair food zote hazina muda wa kuzalishwa na muda wa mwisho wa matumizi
yake". Amesema Mhandisi Manyama.
Pamoja na hayo Mhandisi Manyama
amesema kuwa bidhaa hizo ambazo wamezibaini kuwa na kasoro zinakadiriwa
kuwa na thamani ya Shilingi Milioni 10.
Hata hivyo amesema kuwa
upungufu wa uelewa kwa wauzaji wa bidhaa unasabibisha kuwepo kwa makosa
hayo hivyo TBS itaendelea kuchukua hatua hatua hasa kutoa elimu kwa wale
wote wanaoagiza bidhaa pia wataendelea kuwakumbusha wazalishaji wa
bidhaa za ndani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...