Rais wa TFF, Wallace Karia  (katikati) na mkandarasi  Yixiaobo wa kampuni ya Groupsix International wakionesha mkataba wa ujenzi wa vituo vya mpira  wa miguu vya Dar ea Salaam  na Tanga, mkataba uliosainiwa leo Jijini Dar es Salaam, kulia ni makamu wa  kwanza wa Rais wa TFF Athuman Nyamlani.

Na Agness Francis, Michuzi TV

KATIKA kuendeleza soka la Tanzania na kufikia hadhi ya kimataifa, Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania( TFF) limesaini mkataba na kampuni ya six international Ltd ili kujenga vituo bora vya mpira hapa nchini.

Zoezi hilo la kusaini makubaliano hayo ya ujenzi wa vituo hivyo limefanyika leo Jijini Dar es Salaam katika ofisi za TFF.

Makubaliano hayo yamelenga  mradi huo utakaotekelezwa  katika  Jiji la Dar es Salaam  katika maeneo ya Kigamboni, Kigamboni technical center, pamoja na Mkoani Tanga, Tanga technical center.

Mradi huo utajengwa kwa kutumia fedha za FIFA na unatarajiwa kukamilika  ndani ya miezi  12,  mara baada  ya kuanza kwa ujenzi huo.

Aidha Rais wa TFF  Wallace Karia  amesema kuwa  miradi hiyo inakwenda kwa awamu na matarajio yake ni kuhakikisha kila mkoa unakuwa na vituo hivyo vya mpira.

"Mradi unakwenda kwa awamu, na katika mipango yetu tutahakikisha  kila Mkoa unakuwa na kitu kama hicho,Tutatumia  fedha za wadau wetu mbalimbali pamoja na wale watakaojitokeza pia." Amesema Wallace Karia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...