Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imeibuka mshindi wa pili wa Jumla na kukabidhiwa kikombe cha ushindi katika maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Mwanza Agosti 28 hadi Septemba 5, 2020.
TMDA inashiriki katika maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu juu ya udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi.
Katika maonesho haya hamasa kubwa imewekwa katika umuhimu wa utoaji taarifa juu ya madhara yatokanayo na matumizi ya dawa ma vifaa tiba.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda ma Biashara, Prof. Riziki Shemdoe.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...