Na Mwandishi Wetu

Mgombea ubunge wa tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM) katika Jimbo la Masasi Mjini, lililopo Mkoani Mtwara,Geoffrey Mwambe amewaomba wananchi wa jimbo hilo kumchagua kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu ili aweze kuliongoza jimbo hilo na kuwaletea maendeleo.

Mwambe ambaye aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji(TIC) alisema hayo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Napupa ambapo pamoja na mambo mengine, alisema kuwa, wananchi wa Masasi Mjini wanahitaji kiongozi bora atakayeweza kuwaletea maendeleo wananchi.

Alisema kuwa, kutokana na hali hiyo, ana kila sababu ya kuhakikisha kuwa, anagombea nafasi ya ubunge ili aweze kushirikiana na serikali ili kuhakikisha wanaletaaendeleo.

"Wananchi wa Masasi Mjini wanahitaji kupata maendeleo ya kweli kupitia rasilimali wanazozalisha, ikiwamo kilimo cha mazao ya korosho, ufuta, choroko na mbaazi, hivyo basi ikiwa watapata masoko ya uhakika wanaweza kuuza mazao yao na kupata fedha ambazo zitawasaidia kupata maendeleo," alisema Mwambe.

Aliongeza kuwa, kutokana na hali hiyo, atahakikisha anashirikiana na serikali ili waweze kutafuta masoko ya uhakika ambayo yatawasaidia kuuza mazao yao na kupata faida.

Alisema lakini pia, atahakikisha anaboresha  miundombinu ya barabafa ili wakulima waweze kurahisisha usafirishaji wa mazao yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...