Na Lusajo Frank, DSJ
WASHIKA mitutu wa Jiji la London Arsenal the Gunners, wamefanikiwa kutinga katika hatua ya robo fainali baada ya kuibamiza Liverpool kwa mikwaju ya penati 5-4.
Timu hizo zilitoshana nguvu kwa sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90, na kuamuliwa kwa mikwaju ya penati.
Mchezo huo uliopigwa majira ya saa tatu na dakika arobaini na tano usiku, saa za afrika mashariki katika dimba la Anfield.
Arsenal inatinga hatua ya robo fainali, itaivaa Manchester city iliyotinga hatua hiyo baada ya kuibutua Burnley
bao tatu kwa sifuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...