Na Said Mwishehe, Michuzi TV

CHAMA cha Siasa nchini cha Tanzania National League for Democracy (NLD) kimepinga kauli ya Makamo Mwenyekiti wa chama hicho upande wa Zanzibar Hamadi Hemedi ambaye aliyedai Chama hicho kitamuunga mkono mgombea wa urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharifu Hamadi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28,2020.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Chama hicho Tanzania Bara Tozy Matwanga, amesema Makamu huyo mwenyekiti amekiuka utaratibu ,hivyo wanatarajia kumuita kwenye kika cha Kamati Kuu kwa ajili ya kumpa nafasi ya kujieleza.

"Kamati Kuu ya NLD watakaa kikao kwa ajili ya kumpa nafasi Hemedi ili aweze kujieleza kwa sababu gani ametangaza kumuunga mkono Maalim Seif bila kuwashirikisha uongozi wa chama hicho.

"Msimamo wa Chama chetu kwa upande wa Zanzibar tunaye mgombea urais Mfalme Hamisi Hassan na ndio tunamuunga mkono na kuhakikisha anashinda uchaguzi mkuu mwaka huu,"amesema na kuongeza NLD hawana mpango wa kushirikiana na vyama vyengine kama ilivyokuwa katika uchaguzi wa mwaka 2015.

Amesema kwasababu hawaoni faida zaidi ya kuwanufaisha baadhi ya watu huku akibainisha  kwa sasa Mwenyekiti wa Chama cha NLD ni Taifa ni Mfalme Hamisi Hassan na si Oscar Makaidi kama ilivyokuwa inafahamika na watu wengine.

Kuhusu mwenendo wa kampeni za uchaguzi mkuu,Matwanga amesema kuna baadhi ya wagombea wanatoa lugha zinazoashiria uvunjifu wa amani,hivyo amewaomba wananchi kuwa nakini kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa amani na salama.

Ameongeza kwamba hakuna sababu ya kuwasikiliza wanaohubiri uvunjifu wa amani na kusisitiza ni jukumu la watanzania wote kuwapuuza wanaohubiri uvunjifu wa amani."Watanzania tujiepushe na wanasiasa wanaotumia lugha za uchochozi katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu."

Kuhusu mgombea urais wa CCM Dk.John.Magufuli, amesema NLD inaheshimu sheria za Uchaguzi Mkuu, hivyo hawawezi kutoa kauli ya kusema wanamuunga mkono.mgombea urais wa Chama kingine lakini anachoweza kueleza wanampongeza Dk.Magufuli kwa kazi kubwa ambayo anefanya ya kuleta maendeleo pamoja na ujenzi wa miundombinu ya barabara.

"Tunafahamu hakuna mahali tunataka kusifu au kupongeza kazi ambazo Rais Magufuli amefanya,hivyo tunampongeza kwa kuboresha miundombinu na ukweli miundombinu ya barabara ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi,"amesema Matwanga.

Katibu Mkuu wa Chama cha NLD Tanzania Bara Tozy Matwanga akifafanua jambo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...